Recent comments

Tofauti kati ya 32-Bit OS na 64-Bit OS

Mifumo endeshi ya Windows yenye 64-Bit ilitengenezwa ili kusapoti kiwango kikubwa cha RAM ukilinganisha na ile ya 32-Bit. Software kubwa kama Autocard, Photoshop, Cinema 4D pamoja na Magemu yanahitaji kiwango kikubwa cha cha RAM hasa inayotolewa na mfumo endeshi mpaka kufikia 16 exabytes. Kiwango cha RAM za kupachika kinachohitajika hutegemea sana na aina ya motherboard unayotumia.
Kiwango kidogo cha RAM kinachohitajika ili mfumo wa 32-Bit ufanye kazi vizuri ni 1GB wakati ule wa 64-Bit unahitaji 2GB na kuendelea.  Hii ipo wazi kwani 64-Bit ina regista kubwa hivyo kiwango kikubwa cha RAM kitahitajika. Kama unahitaji kupata matokeo mazuri kutoka kwenye kompyuta ya 64-Bit ni bora uwe na RAM inayoanzia 4GB na kuendelea na kwa wale wa 32-Bit ni bora uwe na RAM inayoanzia 2GB na kuendelea.
Kitu cha msingi unachotakiwa kufahamu ni kwamba 32-Bit Processor inafanya kazi vizuri tu katika kompyuta ya 64-Bit processor ila hautofurahia uzuri wa processor hii. Unachotakiwa kufanya ni kuweka 64-bit OS. Pia software na Drivers zinahitajika kuwa za 64-bit ili kupata kasi nzuri.
Tatizo kubwa la 64-Bit OS ni kwamba software nyingi zinagoma kufanya kazi na mifumo endeshi hii kwa sababu bado madeveloper hawajatengeneza software za kutosha katika soko zinazoendana na mfumo huu, lakini usihofu kwa sasa utapata software zote za muhimu za 64-bit, mfano Mozila Firefox wameanza kutengeneza kiinjari cha 64-bit hapo Desemba mwaka jana.
Kwa ushauri, kama unaenda kununua kompyuta kwa sasa ni bora ukanunua ya 64-Bit ili kuendana na mazingira ya teknolojia yanayobadilika kwa kasi hivi sasa na ili kupata faida zaidi ya kile unacholipia.

Tofauti kati ya 32-Bit OS na 64-Bit OS Tofauti kati ya 32-Bit OS na 64-Bit OS Reviewed by Positive thinking on 3:56 AM Rating: 5

1 comment

Recent