Recent comments

Cloud Computing na faida zake, Ubaya wake na Ushauri wake


Kwa urahisi kabisa cloud computing ni kitendo cha kuhifadhi data au applications zako kwenye server maili kadhaa kutoka ulipo wewe. Kila unapotaka kuzitumia unaingia kwenye Internet na kuingia kwenye account yako na kuzikuta hapo. Hakuna haja ya kuzihifadhi kwenye komputa yako, unakuwa unazipata na kuzitumia pale unapozihitaji tu siyo tu kwa kutmia komputa bali kwa kutumia kifaa chochote kama simu ya mkononi, tablets, notebook, n.k. Hii inamaanisha una uwezo wa kuzitumia data zako wakati wowote na mahali popote ulipo. Watu wengi na makampuni mengi yanajiingiza kwenye mfumo huu kwa sababu ya urahisi wake. Kwa kutumia cloud computing hauhitaji tena komputa yenye storage capacitykubwa sana nyumbani kwako, kumbuka data zako zinahifadhiwa mahali pengine kabisa. Hii inaleta urahisi kwa sababu hununui komputa ya ghali sana. Pia kumbuka komputa inatumia umeme hivyo unakuwa unatumia umeme mdogo zaidi kama uko kwenye cloud ukilinganisha na mtu anayehifadhi kila kitu kwenye system yake nyumbani. Kwa makampuni gharama za kununua hardware zinapungua sana.
Japokuwa tunayazungumzia mazuri ya cloud computing, si kweli kwamba basi tusahau mfumo tuliouzoea wa kuwa na komputa na kila kitu ndani yake nyumbani kwako. Ukweli ni kwamba unahitaji Internet connection kila mara unapotaka kutumia data zako au applications services. Hii ni mbaya hasa kwa nchi kama za kwetu Africa ambapo kuna matatizo ya Internet na umeme. Tatizo lingine kubwa ni data security. Wakati makampuni mengi yanayohifadhi data zetu kwenye serves zao wanatuhakikishia kwamba watazihifadhi data zetu vizuri, usalama wake ni mdogo kwa maana anayezihifadhi ni mtu mwingine na wala huwezi kugundua ikiwa atazitumia au kuziangalia data hizo bila ruhusa yako. Hii ni hatari zaidi kwa makampuni kwa maana siri zao za kibiashara zinakuwa zinahifadhiwa na mtu mwingine mahali pengine.
Ushauri

Ni vizuri kama tunataka mafanikio, kuhakikisha kabla ya kujiingiza kwenye teknolojia hii, basi tunajua faida na madhara yake. Elimu ya teknolojia hii itakusaidia kufahamu kama unahitaji cloud computing kwa matumizi yako au ya biashara yako. Kuna wale wanaopendelea urahisi wa kuweza kuzi-access data zao wakati wowote na mahali popote (flexibility and mobility) lakini wapo wale wanaopendelea kuwa na uhakika kwa kuhifadhi data zao wenyewe (ownership and control).
Cloud Computing na faida zake, Ubaya wake na Ushauri wake Cloud Computing na faida zake, Ubaya wake na Ushauri wake Reviewed by Positive thinking on 3:05 AM Rating: 5

No comments

Recent