Recent comments

YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO



YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO
(basi roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani wakiyasikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya shetani……wakiwazuia watu wa sioe na……1Timotheo4:1-5)

SABABU ZA MSINGI ZA KUYAFAHAMU MFUNDISHO YA UONGO

1.   Ili tusiwe na kuishindania imani ambayo watakatifu wamepewa mara moja tu (Yuda1:3)
2.   Ili tuweze kuvipiga vita vizuri vya imani na kuilinda imani mpka wakati tutakapomaliza mwendo ulioko mbele yetu (2Timotheo4:7)
3.   Ili tusiwe watoto wachanga na kutupwa kule na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu za kigeni na mafundisho ya kishetani (Efeso4:14)
4.   Ili tusichukuliwe na mafundisho ya kigeni yaliyo na mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya shetani (Waebrania13:9 ,1Timotheo4:1)

MAFUNDISHO YA UONGO NI YAPI?

Lolote lililo kinyume na kweli ya Mungu yaani biblia linatokana kwa Baba wa uongo ambaye ni Ibilisi (SHETANI). Kwa hiyo , tunatakiwa kuelewa kuwa shetani ni Baba wa uongo na kwake kamwe haitoki kweli bali ni uongo(Yohana8:44) Kwa hiyo ili shetani afanikiwe kupata watu atakaokwenda nao motoni yaani Jehanamu yeye shetani amebuni ya kuwaletea mafundisho ya uongo yaliyo nje ya kweli Mung(Wakolosai2:8)

JE! UTAJUAJE KUWA HAYA NI MAFUNDISHO YA UONGO?

Kwa hiyo tutaweza kufahamu kuwa haya ni mafundisho ya uongo ni kupitia neon la Mungu (BIBLIA) , lolote lilo kinyume na  neno la Mungu latoka kwa Shetani. Hivyo tukitafuta kutoka katika kitabu cha Bwana (BIBLIA) kwa njia ya kufundishwa mafundisho kama hivi tutaweza kuyafahamu mafundisho ya uongo (Isaya34:16)

Kwa sababu ya kutokuwa tayari kufundishwa ndiyo maana wengi wamejikuta wakiingia katika mafundisho ya neno la Mungu. Hivyo tutafute kujifunza toka katika neno la Mungu sio hadithi za wazee na za uongo miyume na watakatifu waliotangulia hawakutafuta kweli toka katika hadithi za wanadamu zilizotungwa (2Petro1:16 , 2Petro2:1-3 ,Wakolosai2:8 ,Efeso5:6-8 ,Marko7:6-8,13). Kwa hiyo tukitaka kuyafahamu mapenzi ya Mungu katika kila jambo lazima tuyachunguze maandiko matakatifu (BIBLIA) inasema nini na wala sio hadithi za wazee (Matendo17:11 , Mathayo22:29 ,Zaburi119:105)

YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO
Baada ya kuokoka ni vizuri kuyaahamu mafundisho ya uongo na mashetani ili upate kuitetea imani yako na kulinda wokovu wako ulioupokea kutoka kwa YESU KRISTO.

A.  KUWAZUIA WATU WASIOE (1Timotheo4:1-3)

Kwa hiyo hakuna mahali popote katika biblia ambapo watu Wamezaliwa wasioe, ila tunaona Mungu ametoa agizo la watu kuoa ili wapate kuijaza nchi (Mwanzo2:18-24, Mwanzo1:27-28). Mtume Paulo alisema mtu akiweza kukaa kama yeye kwa ajili ya Bwana Yesu ni vema , lakini haikuwa na maana aliwazuia watu wasioe (1Wakorintho7:8-9) kwa hiyo moja ya sifa zaa msingi  kwa kiongozi wa kanisa ni kuona kwa hiyo nizuri wachungaji ,makasisi , mapadri , wazee/walehi  , mashemasi  na wengineo wakaoa (1 Timotheo3:1-2

B.   KUABUDU SANAMU (Kutoka20:4-5)

Kwa hiyo kuabudu sanamu ni moja mafundisho ya uongo nay a kishetani ambayo sisi kama watoto wa Mungu tunatakiwa kuwa mbali sana mahali wanapofundisha mafundisho hayo(WAlawi26:1 , Kumbukumbu4:16-19 , Isaya31:7-1 , Wakorintho10:14-22 , Yohana5:21)

C.   KUPINGA WOKOVU(Marko16:15-16, mathayo28:19-20)

Mojawapo ya mafundisho ya uongo ni kupinga kuwa hakunakuokoka yaani wokovu na kwamba kuokoka ni kule Mbinguni(Waebrania9:27 , Yohana3:16 , 1Timotheo1:15 , Warumi10:9-10,13)

D.  KUBATIZA WATOTO WADOGO NA WALE WASIOAMINI (Mathayo10:14-16)

Kubatiza watoto wadogo ni moja ya mafundisho ya uongo ya shetani kwa sababu hata Bwana Yesu Kristo mwenyewe hakuagiza tubatize watoto wadogo ila alisema watoto wadogo kama hawa ufalme wa Mbinguni ni wao hivyo Yesu aliagiza watoto wadogo wabarikiwe na kuwekwa wakfu kwa bwana mbele ya madhabahu ya Mungu(Luka2:27-34)

E.   KUOMBA WAKFU NA KUENDESHA IBADA KWA AJILI YA WAFU (Kumbukumbu18:9-12 , Kumbukumbu14:1-2)

Mafundisho ya kuomba wafu na kuendesha ibada kwa ajili ya wafu ni mafundisho ya uongo nan i mafundisho ya kishetani (Kumbukumbu14:12)
F.    HADITHI ZA KIZEE (2Petro1:16 , 2Petro2:1-3)

Kwa hiyo kuomba kupitia rozali , maji ya Baraka ni mafundisho ya mashetani na hadithi zakizee. Hakuna mahali popote ndani ya biblia inaposema tuombe kupitia rozali ila hiyo hadithi ni  mawazo ya mtu aliyeota ndoto na sio neno la Mungu

YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO YAFAHAMU MAFUNDISHO YA UONGO Reviewed by Positive thinking on 2:30 PM Rating: 5

1 comment

  1. Nafikiri mafundisho kwenye Biblia kadri ya nukuu sio ya uongo bali tafasiri ndizo za uongo.nilipofungua ambatanisho hili nikakutana na kichwa cha habari "yafahamu mafundisho ya uongo" nilitegemea kuyaona hayo mafundisho ya uongo badala yake nakutana na mafungu ya biblia yenye mafundisho sahihi.ukianza kutaja hayo mafundisho ndipo ufanye reference kwa kutumia hivyo vitabu utakuwa umetusaidia sana wasomaji dhidi ya mkanganyo.asante

    ReplyDelete

Recent